Featured

    Featured Posts

    Social Icons

    .
Loading...

LIVERPOOL YAIGALAGAZA MANCHESTER UNITED

 Liverpool manager Jurgen Klopp punches the air with delight after Firmino's strike doubled their first-leg advantage
Liverpool vijogoo vya Anfield  wameanza vyema kampeni zao kwenye michuano ya Europa League hatua ya 16 bora baada ya kuiangushia kipigo Manchester United cha bao 2-0 kwenye uwanja wa Anfeild jana usiku.
 Liverpool fans show their passion for their club ahead of kick-off in their Europa League first-leg encounter
Ulikuwa usiku mzuri kwa mashabiki wa Liverpool usiku wa jana na kuwa mchungu kwa Mashabiki wa Manchester United waliosafiri kuja kuiangalia timu yao wakizani wataendeleza ubabe wao kwa Liverpool lakini haikuwa hivyo.
 Firmino (right) fired home Liverpool's second goal during the Europa League first leg encounter with this left-footed strike
  Goli la pili lililoimaliza Manchester United usiku wa jana likifungwa na Firmino.
.....
Kikosi cha Jurgen Klopp kilitawala mchezo huo kwa asilimia kubwa ya mchezo huo wa kwanza kati ya timu hizo za Premier League giants huku kocha huyo wa kijerumani akifurahia ushindi wake dhidi ya United.


Daniel Sturridge aliipa Liverpool goli la kuongoza dakika ya 15 kwa mkwaju wa penati baada ya Memphis Depay kumfanyia madhambi Nathaniel Clyne kwenye eneo la hatari penati ambayo imezua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii wadau wakikosoa kwamba ilikuwa ni nje ya penalty box.

Liver vs Man U 1
Roberto Firmino akaongeza bao jingine kwa shuti kali la karibu zikiwa zimesalia dakika 17 pekee mchezo huo kumalizika.


United haikutengeneza hata nafasi moja ya kufunga, ubora wa golikipa wao David de Gea  ndiyo umeikoa United kuchezea idadi kubwa ya magoli kwenye mchezo huo baada ya mlinda mlango huyo wa Hispania kuokoa michomo mingi.

Rekodi zilizowekwa kwenye mchezo huo:
Liver vs Man U 2
  • Manchester United hawajashinda mchezo wowote wa ugenini kati ya michezo yao sita iliyopita kwenye hatua ya moano ya michuano ya Ulaya, wamepoteza michezo mitano kati ya hiyo. 
  • United imepata clean sheet moja kwenye mechi 10 walizocheza kwenye uwanja wa Anfield kwenye mechi za mashindano yote.
  • Daniel Sturridge amefunga magoli matano na ku-assist goli moja kwenye mechi saba dhidi ya United kwenye mashindano yote.
  • United wamepigiwa mashuti nane on target dhidi ya Liverpool, mashuti mengi zaidi kuziuwa na klabu hiyo ndani ya mechi moja msimu huu.
  • Roberto Firmino amefunga magoli matatu mfululizo kwa mara ya kwanza kwenye mechi za Liverpool.
author

This post was written by: Author Name

Your description comes here!

Get Free Email Updates to your Inbox!
© Copyright Udaku Kijiweni
Back To Top