Siamini kuwa watu wanajazba sana.,kwa kuwa najiuliza jazba yao inatokana na nini..? na sioni sababu iliyo dhahiri.,bali naamini ni mpango wa maksudi unaolenga kuzorotesha shughuli za bunge na kuacha kujadili yale ya msingi kwa kudeflect ajenda ya bajeti kuwa ni kampeni za kukipamba chama fulani na kukidharau na kudunisha chama kingine.
Ni ipi hoja Bajeti..? ama udhaifu wa Rais, au upuuzi wa CCM kama mnyika anavyodai..? Maneno haya ni ya kuudhi yanalenga kuamsha hisia za ukali na jazba ya watu ili wajibu hayo na kuacha mjadala wa msingi. Ni namna ya ku-sabotage
utendaji wa serikali na mhimili yake ikiwemo bunge..,ikiwa kazi ya bunge kwa mujibu wa katiba ni kuisimamia serikali na kuishauri..,siioni kazi hii ikifanyika ipasavyo bali naona kuwa bungeni kumegeuka kuwa uwanja wa kampeni na malalamiko..,
Niliwahi kusema hapo mwanzo kuwa wabunge waache kulalamika na watumie fursa ya bunge katika kushauri, kukosoa na kuirekebisha serikali na kuisimamia.
Mnyika amepotoka na analenga kupotosha wengine.,ni vema akijirekebisha na kutenda si kwa mihemko na hisia bali kwa uhalisia na uzalendo.

This post was written by: Author Name
Your description comes here!
Get Free Email Updates to your Inbox!
Filed Under:
Siasa
on Tuesday, June 19, 2012