Loading...
Home » Posts filed under SHILOLE
Shilole na Nuhu Mziwanda Basi Tena..Walivyoringishiana Wachumba Mpya Siku ya Valentines Day..
Kama ulikuwa ni msiba wa ‘penzi’ basi arobaini imeisha na sasa maisha
yanaendelea kwa wasanii wa Bongo fleva, Shilole na Nuh Mziwanda ambao
uhusiano wao umekufa na kuzikwa kabisa.
Wiki chache baada ya couple ya ‘shiwanda’ kuvunjika, na juhudi za wadau mbalimbali kutaka kuwapatanisha kugonga mwamba (soma hapa), inavyoonekana Nuh na Shishi kila mmoja ameamua kuendelea na maisha yake kwa kufungua ukurasa mpya wa mapenzi tena kwa vitabu tofauti...
Siku ya Valentines Day Kwao ilikuwa mashindano kila mmoja akiwa busy kupost picha akiwa na au jipya....Tazama picha: Upande wa Nuh Mziwanda naye ameanza kupost picha za msichana mwingine mrembo anayetumia jina la Erah Erah kwenye Instagram, ikiwa ni pamoja na picha walizopiga pamoja kama couple, na mrembo huyo kupost pia kwenye ukurasa wake.
Wiki chache baada ya couple ya ‘shiwanda’ kuvunjika, na juhudi za wadau mbalimbali kutaka kuwapatanisha kugonga mwamba (soma hapa), inavyoonekana Nuh na Shishi kila mmoja ameamua kuendelea na maisha yake kwa kufungua ukurasa mpya wa mapenzi tena kwa vitabu tofauti...
Siku ya Valentines Day Kwao ilikuwa mashindano kila mmoja akiwa busy kupost picha akiwa na au jipya....Tazama picha: Upande wa Nuh Mziwanda naye ameanza kupost picha za msichana mwingine mrembo anayetumia jina la Erah Erah kwenye Instagram, ikiwa ni pamoja na picha walizopiga pamoja kama couple, na mrembo huyo kupost pia kwenye ukurasa wake.
Filed Under:
SHILOLE
on
NUHU MZIWANDA AFUNGUKA 'SHILOLE HAKUWA MKE MZURI KWANGU NDIO MAANA NIMEFUTA TATTOO YAKE

Msanii
Nuh Mziwanda amefunguka baada ya kuachana na mwandani wake Shilole, na
kusema kuwa Shilole hakuwa mtu mzuri kwake, ndiyo maana ameamua kufuta
hata tatoo ya jina lake aliyoichora.
Nuh
ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo
kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba wakati yupo kwenye
mahusiano na Shilole alishindwa kuonesha undani wake, ambao amekuja
kuujua baada ya kuachana na penzi kuisha.
“Baada
ya mapenzi kuisha mi nimekuwa adui yake, amehack acount yangu ya
instagram najaribu kuwacheki wa kurudisha acount yangu wanashindwa
kunirudishia anabana kila sehemu, kuna vitu ananifanyia vidogo vidogo
ambavyo nimefanya kugundua kuwa hakuwa mwanamke mzuri kwangu, alikuwa
anashindwa kuonesha true colour yake nimekuja kuijua baada ya kuachana
naye”, alisema Nuhu.
Pia
Nuh Mziwanda amesema iwapo wangeachana kwa amani na Shilole
asingelazimika kuifuta tatoo hiyo, kwani ni ukweli usiopingika kwamba
amemsaidia katika maisha yake.
“Mi
ningeiacha tatoo kama Shishi ningeachana nae poa, kila mtu na maisha
yake fresh tukionana tunasalimiana hakuna noma, lakini mwenzangu kwenye
interviews anasema, akiitwa kwenye interview anaongea hiki kwamba mimi
sina kitu, sijui nashindwa kusurvive nakula magengeni, anaongea vitu
vingi ambavyo anajaribu kutoa fan base yangu, angekuwa mtu mzuri baada
ya kuachana naye tatoo ningeiacha kwa sababu ningejua bado kabaki kuwa
rafiki yangu na ni mtu ambaye alinisaidia”, alisema Nuh.
Pamoja
na hayo Nuh amesema yeye binafsi hana chuki na msanii huyo ambaye
alikuwa naye kwenye mahusiano, na kwa sasa ana mahusiano mengine ambayo
asingependa kuyaweka wazi.
Mimi
sina ubaya na Shishi , sina ugomvi naye na wala sitaki kufikiria kuja
kuwa na bifu naye, nipo kwenye mahusiano lakini siwezi kuweka wazi
mahusiano kwenye mitandao ya kijamii, sababu ni mke wangu yuko kwenye
moyo wangu, hayupo instagram wala kwenye mitandao ya kijamii”, alisema Nuh.
Filed Under:
SHILOLE
on Monday, February 8, 2016
STAA NUH MZIWANDA AMTUPIA MANENO HAYA SHISHI BABY
STAA
wa Wimbo wa Msondo Ngoma, Naftari Mlawa ‘Nuh Mziwanda’, anasemekana
amemwangukia kwa mara nyingine aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohamed
‘Shilole’ kwa kumtaka warudiane.
Kwa
mujibu wa chanzo chetu, Mbongo Fleva huyo amekuwa katika wakati mgumu
tangu alipoachana na Shilole hivyo kulazimika kumpigia simu na
kumwandikia ujumbe wa maneno akimuomba amsamehe na warejeshe penzi lao
kama ilivyokuwa zamani.
“Ndugu
yangu nikikwambia kuwa, Nuh maji yamemfika shingoni basi huna haja ya
kuuliza mara mbili namna yalivyomfika kwani, juzikati nilikuwa naongea
na Shilole akalalamika kwamba, jamaa huyo ameanza tabia ya kumpigiapigia
simu akimwomba warudiane jambo ambalo Shilole analitolea nje,” kilisema
chanzo hicho.
Baada
ya kupenyezewa ubuyu huo, paparazi wetu alimtafuta Shilole kwa nia
njema ya kutaka kujua ukweli wa madai hayo ambapo alisema ishu hiyo ipo
ila hawezi kuanika wazi.
“Suala
la Nuh kwa sasa sitaki kuendelea kuongea kwani nitakuwa nampigia debe
mtu na kazi hiyo niliifanya sana. Unachotakiwa kujua kutoka kwangu ni
kwamba mimi naendelea kupigania maisha tu ili niweze kusonga mbele na
hapa nipo kipesa zaidi hivyo sina tena muda wa kuendelea kumpa nafasi
bwana wa aina yeyote kwani hapo nyuma maisha yangu yalirudi nyuma hatua
nyingi sana,” alisema Shilole.STAA wa Wimbo wa Msondo Ngoma, Naftari
Mlawa ‘Nuh Mziwanda’, anasemekana amemwangukia kwa mara nyingine
aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ kwa kumtaka warudiane.
Kwa
mujibu wa chanzo chetu, Mbongo Fleva huyo amekuwa katika wakati mgumu
tangu alipoachana na Shilole hivyo kulazimika kumpigia simu na
kumwandikia ujumbe wa maneno akimuomba amsamehe na warejeshe penzi lao
kama ilivyokuwa zamani.
“Ndugu
yangu nikikwambia kuwa, Nuh maji yamemfika shingoni basi huna haja ya
kuuliza mara mbili namna yalivyomfika kwani, juzikati nilikuwa naongea
na Shilole akalalamika kwamba, jamaa huyo ameanza tabia ya kumpigiapigia
simu akimwomba warudiane jambo ambalo Shilole analitolea nje,” kilisema
chanzo hicho.
Baada
ya kupenyezewa ubuyu huo, paparazi wetu alimtafuta Shilole kwa nia
njema ya kutaka kujua ukweli wa madai hayo ambapo alisema ishu hiyo ipo
ila hawezi kuanika wazi.
“Suala la Nuh kwa sasa sitaki kuendelea kuongea kwani nitakuwa nampigia debe mtu na kazi hiyo niliifanya sana.
Unachotakiwa
kujua kutoka kwangu ni kwamba mimi naendelea kupigania maisha tu ili
niweze kusonga mbele na hapa nipo kipesa zaidi hivyo sina tena muda wa
kuendelea kumpa nafasi bwana wa aina yeyote kwani hapo nyuma maisha
yangu yalirudi nyuma hatua nyingi sana,” alisema Shilole.
Chanzo:GPL
Filed Under:
SHILOLE
on Friday, February 5, 2016
SHILOLE AKANA KUSAFIRISHA MADAWA YA KULEVYA NJE YA NCHI LAKINI AKIRI KUSHAWISHIWA
Shilole amekanusha kujihusisha na kusafirisha madawa ya kulevya katika
safari zake za nje lakini amekiri kuwahi kushawishiwa kufanya hivyo.
Muimbaji huyo alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EATV kuwa alikataa mtego huo kwakuwa hakupenda kuhatarisha maisha yake.
“Kiukweli ushawishi upo niache kusema uongo lakini kwa sababu binafsi na akili zangu timamu na najua nini nafanya basi huwa naweka tamaa pembeni na kuangalia kitu ambacho kina mwendelezo na maisha yangu,” alisema.
“Nikiwaangalia watu halafu nikiangalia mpenzi wangu ninavyompenda nimwache hivi hivi, roho inauma pamoja na watoto wangu, nawapenda sana. Halafu wananipa matumaini kwa sababu wana akili sana shuleni,” alisisitiza.
Muimbaji huyo alikiambia kipindi cha Planet Bongo cha EATV kuwa alikataa mtego huo kwakuwa hakupenda kuhatarisha maisha yake.
“Kiukweli ushawishi upo niache kusema uongo lakini kwa sababu binafsi na akili zangu timamu na najua nini nafanya basi huwa naweka tamaa pembeni na kuangalia kitu ambacho kina mwendelezo na maisha yangu,” alisema.
“Nikiwaangalia watu halafu nikiangalia mpenzi wangu ninavyompenda nimwache hivi hivi, roho inauma pamoja na watoto wangu, nawapenda sana. Halafu wananipa matumaini kwa sababu wana akili sana shuleni,” alisisitiza.
Filed Under:
SHILOLE
on Wednesday, November 11, 2015